Na Karoli Vinsent
HOFU ya Mabilioni ya walipa
kodi kupotea bure kutokana na Mchakato wa katiba mpya yabainika,hii inatoka Hotuba
ya Rais Jakaya Kikwete Wiki iliyopita bungeni huku akionekana kufanya usaliti mkubwa Tume
ya Mabadiliko ya Katiba huku akiyafuata matakwa ya chama chake cha CCM.
Hofu hii ya mabilioni ya
Wananchi walalahoi kupotea inatoka na kupata katiba mpya yenye kuwanufaisha
viongozi kama Rais Kikwete na Chama chake cha CCM na sio wananchi walalahoi wa Tanzania.
Rais Kikwete juzi wakati
anahutubia Wajumbe bungeni alionekana wazi kiongozi huyo kuwasaliti
watanzania,huku akishindwa kuwaachia wajumbe ambao zaidi ya 600 kuamua hatma ya
katiba badala yake yeye ndio kuamua mchakato mzima wa katiba.
Wachambuzi mbalimbali
waliozungumza na mwandishi wa Mtandao huu wengi walihoji hata uwezo wa kiongozi
huyo mkubwa wa nchi kitaaluma, baada ya kuonekana wazi kuboronga katika
mchakato mzima wa katiba.
Mchambuzi ambaye ametoka Chuo
Kikuu cha Dodoma Seiph Yahaya ambaye kwa upande wake alimshangaa Rais Kikwete
kuonekana kufanya usaliti mkubwa kwenye tume iliyotumia pesa nyingi za walipaka
kodi na kuonekana sawa na bure.
Yahaya ambaye ni Msomi wa
Shahada ya juu masuala ya Sayansi ya siasa alisema ni Dhahiri Shairi Rais
Kikwete hana nia njema kwa watanzania kupata katiba mpya badala yake alikurubuka
tu kuanzisha mchakato huu,
huku akisahau kwamba
watanzania walimwamini kama kiongozi
atakayekumbukwa kwenye historia lakini kwa ishara hii amejichafua kwa wananchi alisema mchambuzi
huyo.
Usaliti wa Rais Kikwete
kwenye mchakato huu Wa katiba mpya ulionekana wazi wakati alipokuwa anateua
wajumbe 201,ambapo katika uteuzi huu
aliwajaza makada wenzake wa Chama cha Mapinduzi,huku akiwaacha watu muhimu
kutoka kwa wananchi.
Wamejazana bungeni kana kwamba wanatunga
katiba ya chama chao, wanataka kuumeza mchakato huu. Sina shaka tuendako si
kwema.
Najua wanasiasa wengi hivi sasa wanawaza madaraka tu ndiyo maana hata Rais Kikwete hataki wananchi wawe na nguvu ya kuwaondoa wabunge wao wanaovurunda.
Najua wanasiasa wengi hivi sasa wanawaza madaraka tu ndiyo maana hata Rais Kikwete hataki wananchi wawe na nguvu ya kuwaondoa wabunge wao wanaovurunda.
Wanataka katiba itungwe kulinda masilahi yao na wala si ya nchi.
Huu ni udhaifu mkubwa sana!
Je Rais Kiwete ulivyokuwa
unawaambia Makada wa Chama chako wajiandae kisakrojia kutokana na mchakato huu
wa katiba kumbe hata wewe ulikuwa ujajiandaa kisakrojia ndio maana umeamua kuvuruga
mchakto mzima wa katiba.
Je hivi unataka tuanze kumwamini Mwanasheria
Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, alishatuambia mapema kuwa hakuna haja ya
kuandika Katiba mpya bali tuiwekee viraka hii tuliyonayo, huyu leo hii ni
miongoni mwa wanaosimamia uandikwaji wa Katiba mpya, je, lini ameona kuna
umuhimu wa kuwa na mpya?
Aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina
Kombani, alipinga mchakato kuandika Katiba mpya lakini hivi sasa naye yumo
bungeni, anashiriki katika kile asichokiamini.
Naandika makala hii kwa uchungu huku nikihoji
Makada wa CCM, chama ni muhimu zaidi kuliko masilahi ya taifa, wako tayari
kuuhujumu mchakato wa katiba mpya ilmradi mazingira ya kufanya ujanja ujanja
nyakati za uchaguzi yaendelee kuwepo.
Makada wa aina hii wako tayari kufumbia macho
uvunjwaji wa Katiba ya Muungano uliofanywa na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010 ilimradi chama chao
kiwe salama.
Je hata kwa Tafsiri hii tunahaja ya kumkumbuka
Rais wetu akiondoka madarakani kwa wema?wakati mabilioni ya walipa kodi
yanapotea kutokana na mchakato huu wa katiba mpya?
Nawasubiri hawa wajumbe wa Bunge maalumu la
Katiba, wachanganye akili za kuambiwa na zao, nasubiri kuvunjika kwa Bunge hili
wakati wowote kuanzia sasa.
Najua ni lazima litavunjika tu, ni suala la
muda tu, litavunjika kwa sababu lilianza bila maridhiano, lilianza kwa mguu
mbaya, ambapo wajumbe wengi wamebeba misimamo ya vyama na makundi yao badala ya masilahi ya
taifa.
Tafakari.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni