Jumamosi, 29 Machi 2014

HIVI NDIVYO RAIS KIKWETE NA CHAMA CHAKE WANAVYOTEKETEZA MABILIONI YA WALIPA KODI KUTOKANA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA SOMA KWA MAKINI MAKALA HII

Na Karoli Vinsent
http://umwezi.net/wp-content/uploads/2013/06/Jakaya-Kikwete.jpg
HOFU ya Mabilioni ya walipa kodi kupotea bure kutokana na Mchakato wa katiba mpya yabainika,hii inatoka Hotuba ya Rais Jakaya Kikwete Wiki iliyopita bungeni huku akionekana kufanya usaliti mkubwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba huku akiyafuata matakwa ya chama chake cha CCM.

Hofu hii ya mabilioni ya Wananchi walalahoi kupotea inatoka na kupata katiba mpya yenye kuwanufaisha viongozi kama Rais Kikwete na Chama chake cha CCM na sio wananchi walalahoi wa Tanzania.

Rais Kikwete juzi wakati anahutubia Wajumbe bungeni alionekana wazi kiongozi huyo kuwasaliti watanzania,huku akishindwa kuwaachia wajumbe ambao zaidi ya 600 kuamua hatma ya katiba badala yake yeye ndio kuamua mchakato mzima wa katiba.

Wachambuzi mbalimbali waliozungumza na mwandishi wa Mtandao huu wengi walihoji hata uwezo wa kiongozi huyo mkubwa wa nchi kitaaluma, baada ya kuonekana wazi kuboronga katika mchakato mzima wa katiba.

Mchambuzi ambaye ametoka Chuo Kikuu cha Dodoma Seiph Yahaya ambaye kwa upande wake alimshangaa Rais Kikwete kuonekana kufanya usaliti mkubwa kwenye tume iliyotumia pesa nyingi za walipaka kodi na kuonekana sawa na bure.

Yahaya ambaye ni Msomi wa Shahada ya juu masuala ya Sayansi ya siasa alisema ni Dhahiri Shairi Rais Kikwete hana nia njema kwa watanzania kupata katiba mpya badala yake alikurubuka tu kuanzisha mchakato huu,

huku akisahau kwamba watanzania walimwamini kama kiongozi atakayekumbukwa kwenye historia lakini kwa ishara  hii amejichafua kwa wananchi alisema mchambuzi huyo.